Featured

    Featured Posts

Picha: Collabo ya Diamond Platnumz NE-YO tayari

Picha: Collabo ya Diamond Platnumz NE-YO tayari




Kile kilichosubiriwa kwa hamu na mashabiki toka Diamond na Ne-Yo wakutane Afrika Kusini kwenye tuzo za MAMA 2015 hatimaye kimetimia, ni collabo ya Diamond Platnumz na mwimbaji huyo wa R&B kutoka Marekani.




Diamond kupitia ukurasa wake wa Instagram amemshukuru Ne-Yo baada ya kumaliza kurekodi wimbo huo. Katika picha aliyopost akiwa na Ne-Yo studio, pia anaonekana producer Sheddy Clever ambaye atakuwa amehusika na kazi hiyo.


“Thanks alot my Brother @neyo and the Whole Compound Crew had a great Session, and it was realy nice working with you…can’t wait for the World to hear this Hit Song!! @Diamondplatnumz ft @neyo ….. Cc @sheddyclever @Compoundu @thecorpshow @Jullianl #AfricaTotheWorld”




Dalili za kufanyika kwa collabo hiyo jijini Nairobi zilianza kuonekana siku moja iliyopita baada ya meneja wa Diamond, Salaam kuonekana kwenye picha iliyosambaa mtandaoni akiwa na Alikiba kwenye Coke Studio na kwa mbali akionekana Ne-Yo.



Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Translate

Total Pageviews

Copyright © DIAMOND PLATNUMZ | Blogger Templates | Designed By Code Nirvana