Diamond Platnumz ni msanii ambaye (angalau kwa sasa) haoneshi dalili za kushuka kimuziki hivi karibuni. Tunayo mifano mingi ya wasanii wa Bongo ambao waliwahi kufanya vizuri sana na baadaye kupotea kabisa kwenye ramani ya muziki.
Diamond ambaye ameachia ngoma mpya ‘Utanipenda’ wiki iliyopita ambayo imekuwa gumzo kwa watu wa kila rika, ana akiba ya hits na collabo za maana, ambazo kwa mujibu wa mpiga picha wake zinampa uhakika wa kuendelea kukaa kileleni kwa miaka mingine kumi ijayo.
Collabo zinazosubiriwa kwa hamu ni pamoja na ile ya Diamond na Ne-yo, Diamond na P-Square, Diamond na Usher na zingine.
Post a Comment